Wednesday, February 17, 2016

HIVI NDIVYO KILIMO CHA MATUNDA KINAVYOWEZA KUKUTOA KIMASOMASO..

MIEMBE NA MIPARACHICHI.

Iwapo utatumia miche iliyoungwa/kubebeshwa(Grafted). Miembe  huzaa matunda  baada  ya miaka 2- 3 baada ya kupandwa shambani.Hali kadhalika kwa Maparachichi.Mwembe mmoja huweza kutoa kati ya Matunda 300-800 kwa mwaka,hii hutegemea aina ya mwembe,ukubwa wa mti,ukubwa wa matunda na kiwango cha utunzaji.

Matunda hukomaa baada ya siku 90 hadi 120 tangu kutunga.Mti mmoja wa Mparachichi huzaa matunda 200 hadi 1000 kutegemea umri wa mti,udongo na utunzaji wa shamba na miti yenyewe.

JINSI KITAKAVYOKULIPA.
Kwa hekta moja uliyopanda, ina uwezo wa kubeba miti kuanzia 500 hivi.Tuchukulie miti 500 kama wastani tu, tukichukuwa makadirio ya mti mmoja kwa wastani kuzaa matunda 500,hivyo hekta moja itakuwa na matunda 250,000.Kama utakuwa na hekta mbili tu inamana hapo unahesabu matunda yako 500,000.

Ukifanikiwa kuuza kwa bei ya jumla,tuchukulie Sh.200 kwa kila tunda,hapo utakuwa umejipatia jumla ya Sh.100,000,000.(Milioni 100).

Wakati huo kabla ya kuvuna maembe/Maparachichi,unaweza kuweka shambani kwao mazao ya muda mfupi kama vile matikiti maji,kunde,maharage au matango.

Kwa ushauri/Maoni niandikie 

fabianbalele@gmail.com/ 0768937884.

Exclusive to Fabian Balele..