Friday, January 24, 2014

FURSA ILIYOPO TANZANIA JUU YA UFUGAJI WA NYUKI.






UFUGAJI WA NYUKI.
1) FURSA ILIYOPO TANZANIA JUU YA UFUGAJI WA NYUKI.
2) Maisha ya Nyuki.
3) Nyumba ya Nyuki.
4) Sifa za Eneo linalofaa kwa Ufugaji wa Nyuki.
5) Mavuno.
6) Umuhimu wa Asali
7) Mazao ya Asali
8) Magonjwa yanayotibiwa kwa Asali.
FURSA ILIYOPO TANZANIA JUU YA UFUGAJI WA NYUKI.
Tanzania ina mazingira mazuri ya kuzalisha mazao ya nyuki kwa kuwa kuna mimea mingi ambayo inatoa maua yenye kutoa mbochi na chavua vitu ambavyo huwavutia nyuki na kutengeneza asali.

Katika Tanzania mazao makuu yatokanayo na ufugaji wa nyuki ni asali na nta. Hata hivyo kuna mazao mengi ambayo yanaweza kuzalishwa kutokana na asali na nta.
 
Tanzania tumejaliwa maeneo mengi sana na makubwa yenye misitu minene yenye chavua na nectar kwa wingi, maeneo haya yapo karibu Tanzania nzima hayana matumizi yoyote yale ya ufugaji wa nyuki, kwa nchi nyingi Africa kama vile Ethiopia na nchi nyinginezo ambazo zinasemekana kuongoza kwa ufugaji nyuki zinatamani sana maeneo mazuri tuliyonayo.

Ukizunguka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tabora, Rukwa, Katavi, Kigoma, Singida,Dodoma, Shinyanga na Mikoa mingine mingi, rasilimali hizi za misitu zimebweteka na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa na serikali yetu ya kuwekea mkazo katika kuwekeza kwa ufugaji wa nyuki.

Tusisitize serikali za vijiji kutoa maeneo hayo ya misitu yenye mahitaji ya nyuki kwa vikundi mbalimbali vya wafugaji nyuki ili kuweza kuiboresha na kuiendeleza idara hii ya ufugaji nyuki

Maisha ya Nyuki 
 Nyuki ni mdudu mwenye mabawa manne angavu na mwiba nyuma ya mwili wake anayekusanya mbelewele ya maua kama chakula chake. Aina inayojulikana hasa ni nyuki wa asali wa familia apis. Kuna spishi zaidi za 20,000 zinazojumlishwa na biolojia kati ya nyuki lakini ni wale wa jenasi apis wanaokusanya asali inayovunwa na wanadamu.

Nyuki za asali mara nyingi wanafugwa lakini wengine wanaishi porini na asali yao inakusanywa kwa kuvunja mzinga wao. Katika Afrika kwa jumla sehemu ya asali bado inatokana na nyuki asali wa porini lakini ufugaji nyuki unapanua.

Hapo mwanzo Wanajamii walikuwa wanafuga nyuki kwenye magome ya miti, vibuyu, vyungu, mapango, vichuguu na kwenye miamba. Baada ya muda ufugaji ulipiga hatua kidogo na watu wengi wakawa wanafuga kwa kutumia mizinga iliyochongwa kutoka kwenye magogo ya miti. Ufugaji wa aina hii umedumu kwa karne nyingi kote nchini Tanzania.
Kutokana na uhitaji na ongezeko la matumizi ya bidhaa za nyuki, kulifanyika tafiti mbalimbali ambazo ziliweza kuboresha ufugaji wa nyuki kwa kuwa na mizinga ya kisasa ambayo imewezesha uzalishaji wa asali kuwa mkubwa na kuongeza pato la wafugaji tofauti na ilivyokuwa hapo awali. Tafiti hazikuishia kwenye kuboresha mizinga tu, ila siku hadi siku kunavumbuliwa namna bora zaidi za kuimarisha uzalishaji wa nyuki.
Nyumba ya nyuki.
Hii ni aina mpya ya ufugaji wa nyuki ambapo unaweza kujenga kibanda au nyumba kisha kuweka mizinga idadi unayohitaji.
Ni kwa nini kujenga nyumba au kibanda?
Ø Ni muhimu kufuga nyuki kwenye kibanda au kwenye nyumba kwa sababu inasaidia kudhibiti wizi wa mizinga, pamoja na wanyama wanaokula asali na kudhuru nyuki.
Ø Inarahisisha utunzaji wa mizinga na kuwafanya nyuki wasihame kwenda sehemu nyingine.
Ø Inasaidia watu wengi kujifunza namna nzuri ya ufugaji wa nyuki, ikiwa ni pamoja na watoto, jambo ambalo linafanya shughuli hii kuwa endelevu.
Ø Ufugaji wa aina hii unasaidia kuwakinga nyuki dhidi ya majanga kama vile moto, na mafuriko.
Ø Inawaepusha nyuki na usumbufu unaoweza kuwafanya wasizalishe kwa kiwango kinachotakiwa.
Ø Uzalishaji unaongezeka. Hii ni kwa sababu mizinga inayotumika ni ile ya kibiashara. Mzinga 1 unapata asali kilo 30 sawa na lita 20.

Aina ya nyumba
Unaweza kujenga nyumba yenye upana wa futi 3 na urefu wa futi 9. Nyumba hii inaweza kuchukua mizinga hamsini. Halikadhalika, unaweza kujenga kibanda chenye ukubwa sawa na huo.
PICHA ZA MABANDA TOFAUTI TOFAUTI YA KUFUGIA NYUKI


 Eneo linalofaa
SIFA ZIFAAZO KWA MAENEO YA KUFUGIA NYUKI (MANZUKI)
Eneo lifaalo kwa shughuli za ufugaji nyuki ni lazima liwe na sifa zifuatazo:
Ø (i) Miti, uoto wowote wa asili na mimea mbalimbali kwa mfano mazao ya chakula na biashara, Kusiwe na aina ya mimea ambayo nyuki hawapendi.
(ii) Maji ya kudumu ambayo hutumika kama sehemu ya chakula cha jamii nzima ya kundi la nyuki. Pia maji hutumika kwa kurekebisha hali ya hewa ndani ya mzinga.
Ø (iii) Eneo la shamba la nyuki ni lazima liwe ni salama kwa mizinga, mazao yake, mifugo, binadamu, na mahali ambapo maadui wa nyuki hawapo au wanaweza kudhibitiwa(Ili kuwa na ufanisi mzuri, nyumba hii inafaa kujengwa nje kidogo ya makazi ya watu, Kusiwe na mifugo karibu, Iwe sehemu ambayo watoto hawawezi kufika, Isiwe karibu na njia ambayo watu wanapita mara kwa mara.)

(iv) Kivuli cha kadri na kinga ya upepo ili kuwapunguzia nyuki kazi kubwa ya ubebaji maji kwa ajili ya kupunguza joto. Inafaa kufugia nyuki ndani ya nyumba iliyoandaliwa kwa ajili ya ufugaji wa nyuki(bee-house)

Mawasiliano ya barabara ni muhimu yawepo ili kurahisisha uhudumiaji wa makundi ya nyuki pamoja na mazao yake hadi kufikia sokoni.

Mavuno
Baada ya kujenga nyumba, kuweka mizinga na nyuki kuingia, unaweza kuvuna kwa mara ya kwanza baada ya miezi mitatu. Utaweza kupata mavuno mazuri endapo utavuna kabla nyuki na wadudu wengine hawajaanza kula asali.
Ni muhimu kuhakikisha kuwa wadudu waharibifu kama vile sisimizi, mende na wengineo wanadhibitiwa ili kutokuathiri uzalishaji wa asali. Hakikisha unavuna kitaalamu ili kuepuka upotevu wa asali. Endapo nyuki wametunzwa vizuri na kwenye mazingira mazuri, unaweza kuvuna asali mara tatu kwa mwaka. Katika mzinga mpya nyuki wana uwezo wa kutengeneza masega kwa siku tatu na kuanza uzalishaji wa asali.
Ni nini umuhimu wa asali
• Asali inatumika kama chakula
• Inatumika kama tiba ya magonjwa mbalimbali
• Hutumika kutibu majeraha
• Ni chanzo kizuri cha kipato
• Hutumika katika kutengeneza dawa za binadamu
*Asali inaweza kuhifadhiwa kwa miaka mingi sana bila kuharibika. Hii inatokana na wingi wa dawa maalum iliyo nayo inayofanya isiharibike.
MAGONJWA YANAYOTIBIWA KWA
MATUMIZZI YA ASALI.
1. Ugonjwa wa viungo/maumivu na uvimbe.
2. Kukatika kwa nywele.
3. Ukungu wa miguu.
4. Maambukizo kwenye kibofu cha mkojo.
5. Maumivu ya jino.
6. Helemu (Cholestral).
7. Ugumba
8. Mchafuko wa tumbo.
9. Ugonjwa wa moyo
10. Shinikizo la damu.
11. Kinga ya mwili.
12. Ukosefu wa nguvu za kiumbe.
13. Flu.
14. Umri wa kuishi.
15. Chunusi.
16. Kuumwa na wadudu (kwa washawasha) wenye sumu.
17. Madhara ya ngozi.
18. Kupungua kwa uzito.
19. Saratani.
20. Uchovu mwilini.
22. Harufu mwilini.
23. Kupungua kwa usikivu.

Bidhaa zinazotokana na asali
 Kuna aina nyingi ya bidhaa zinatokana na asali, kwa kutengenezwa na nyuki wenyewe na nyingine zikitengenezwa na binadamu kutokana na tafiti mbalimbali. Miongoni mwa bidhaa hizo ni:
• Asali yenyewe
• Royal jelly : Hii ni aina ya maziwa yanayotengenezwa na nyuki, ambayo hutumika kama tiba.
Gundi: Hii hutumika kutengeneza bidhaa za aina mbalimbali kulingana na mahitaji ya mtumiaji.
Nta: hutumika kutengenezea mishu maa, kulainisha nyuzi, kutengeneza dawa ya viatu, mafuta ya kupaka, pamoja na dawa ya ngozi.




                          SHAMBA LA NYUKI.


                  MZINGA WA KISASA WA NYUKI



 KWA USHAURI NA MAONI.
NIANDIKIE:fabianbalele@gmail.com
                     +255768937884
                              Exclusive to:                                                 balelemwanahabari.blogspot.com

1 comment: