Sunday, March 31, 2013

HIVI NDIVYO TAMASHA LA PASAKA(2013) LILIVYOFANA MOROGORO

Tamasha la Pasaka Mjini Morogoro lililofanyika Jamhuri Stadium limefana Baada ya Waimbaji mabalimabli wa nyimbo za Injili kuonyesha umahili wa hali ya juu walipokua wakitumbuiza kwa nyimbo zao.

Tamasha hilo lililoandaliwa na Qs Mhonda J Entertainment limewashirikisha waimbaji mabalimbali wa Morogoro huku Waimbaji kutoka Dar es Salaam wakihitimisha na kuonyesha umahili mkubwa .

Muimbaji Catherine John kutoka Morogoro akitumbuiza
mwanzo wa Tamasha hilo.
Revina Steven kutoka Morogoro naye akafatia
katika kumwimbia Bwana.
Bahati Bukuku na Stara Thomas wakienda kumtuza Muimbaji Catherine John
Walishindwa kujizuia baada ya Catherine John kuzikosha nyoyo zao na Mashabiki kwa ujumla
JGM Choir Kutoka Mororgoro nao wakafatia.


Haleluya  Choir Kutoka Morogoro wakionyesha manjonjo kwa style mbalimbali katika kumwimbia Bwana.
 Stara Thomas amabye sasa ni muimbaji wa Nyimbo za Injili akifikisha ujumbe wa Mungu kupitia Nyimbo.
Emanuel Mgaya (Masanja)a.k.a Mchungaji Mtarajiwa akimkaribisha Jukwaani Stara Thomas
Masanja kwa sasa amekua akiimba nyimbo za Injili huku akieleza nia ya kua Mchungaji hapo Baadae.
Mkurugenzi wa QS Mhonda J Entertainment(waandaaji wa Tamasha) akimuelekeza Emanuel Mgaya(Masanja) jinsi ya Kuendesha shughuli za Tamasha hilo.


Muimbaji Mkongwe wa nyimbo za Injili Bahati Bukuku akionyesha umahili wake wa kueneza Injili kupitia Nyimbo za Injili.

 Joseph Nyuki akionyesha umahili wake,
alizikosha nyoyo za mashabiki na wapenzi wa Nyimbo za Injili babada ya kulitawala jukwaa kupitia style zake za kipekee kwa Kucheza na kuruka.

Rafiki Gospel Singers kutoka jijini Dar es Salaam waionyesha manjonjo katika kumwimbia Bwana.

Martha Mwaipaja Mwenye Microphone akionyesha umahili wake katika kumwimbia Bwana.
JUKWAANI: Wapenzi wa Nyimbo za Injili waliojitokeza Mjini Morogoro katika Tamasha hilo.




No comments:

Post a Comment