Saturday, March 30, 2013

ONYESHA UZALENDO KWA VITENDO,SISITIZA MATUMIZI YA BIDHAA ZA KITANZANIA("MADE IN TANZANIA) NDIO KAULI YETU.


RASTAFARIAN- MOSSEAH ABRAHAMU Ni mdau mkubwa katika Biashara za Bidhaa mbalimbali za Kitanzania Ndani ya Jiji la Mwanza.

Rasi Mosseah aliifahamisha Blog hii kua alichagua kujihusisha na biashara ya bidhaa za asili kutoka Tanzania kwa kua yeye binafsi anapenda kuitangaza Tanzania na kuuthibitisha uzalendo kwa vitendo.

Alibainisha kua kwa kiasi kikubwa Watanzania hawapendi kununua bidhaa za nyumbani na wamekua wakinunua bidhaa za nje kwa kisingizio cha ubora hali ambayo alidai kua si kweli kua bidhaa zetu hazina ubora bali ni utamaduni mbaya tuliouzoea.

Wadau mbalimbali wamekua wakisistiza kutumia bidhaa zinazotengenezwa nyumbani ili kuimarisha uchumi.

Rasi Abrahamu aliiomba serikali kuwawezesha wadau wote wanaojihusisha na bidhaa za nyumbani kimtaji na kuwaongezea taaluma za kiujasiriamali.





KULIA:Ni baadhi ya wanunuzi  kutoka nyumbani(Tanzania).
Kwa mujibu wa Rasi Abrahamu,Wanunuzi kutoka Nyumbani ni wachache sana ukilinganisha na wanunuzi wa Kigeni.





































KUSHOTO:RASI MOSSEAH ABRAHAMU Akinionyesha baadhi ya bidhaa zinazopatikana katika duka lake la WEUSI WA KALE WAENZI @ ART GALARY



JUU KABISA: NI BIDHAA ANAZOUZA RASI ABRAHAMU



WASILIANA NA RASI MOSSEAH ABRAHAMU KUPITIA    +255   ( 0)767175778
                                                                                                                    ( 0)785978580
                                                                                                                    ( 0)716902246

BARABARA YA KAPRI POINT NDANI YA JIJI LA MWANZA.

No comments:

Post a Comment