Monday, December 28, 2015

SIFA ZA SHAMBA LA NYUKI (MANZUKI)


Kuwapo Kwa mimea inayotoa Maua yanayotoa chakula cha nyuki cha kutosha, Kwa mfano,sehemu yenye misitu, shamba la miti au mazao ya kilimo. Muda wa mimea kuchanua ujulikane kwa mfugaji nyuki ili aweze kupanga muda ambao atawezesha kundi la nyuki kujijenga na kukusanya mazao ya kutosha wakati mimea inapochanua Maua. 

Maji ya kutosha ni muhimu, nyuki huyatumia kupooza kupooza joto ndani ya mzinga, kulainisha chakula na kurekebisha utamu wa asali ambayo hulishwa majana. 

Mahali panapofikia ili kuwezesha usafirishaji wa vifaa na mazao ya nyuki nyakati za uvunaji. 

Umbali wa kilomita tatu kutoka katika makazi ya watu,shule,hospitali na pasiwe mahali ambapo ni mapito ya Mifugo. Inapolazimu kuwa na Manzuki katika maeneo haya ,izungushiwe uzio wenye miti mirefu ili nyuki wanapokwenda nakurudi kutafuta cha kula wapiti juu  ili wasishambulie watu na wanyama. Umbali uliotajwa hapa ni kwa ajili ya nyuki  wanaouma tu. 

Mbali na maeneo ya kilimo kinachotumia kemikali kwa mfano kilimo cha tumbaku na korosho, Manzuki yaanzishwe umbali wa kilometa saba kutoka maeneo hayo. Hii ni kuzuia nyuki wasife kwa kemikali hizo, au kuzuia mizinga isiangushwe na pia kusababisha nyuki washindwe kurudi kwenye mizinga.
Kudhibiti uharibifu kutokana na maadui wa nyuki, wizi wa mizinga na mazao ya nyuki.

Viashiria Vifuatavyo hutumika sehemu mbalimbali kutambua muda wa kuvuna Asali..
i)Mwisho wa Msimu wa mvua na mwanzo wa Kangazi

ii)Maua au matunda ya mmea Fulani kupukutika

iii)Matunda ya mmea mwitu kutokeza

iv) Mazao ya shamabani kukomaa

v)Mng’urumo wa nyuki wakusanyao chakula kupungua

vi)Madume ya nyuki kuonekana yamekufa kwenye mlango ama chini ya mzinga

vii)Kundi la Nyuki kutanda nje ya Mzinga

viii)Gundi nyingi kuonekana katika mlango na matundu ya Mzinga

ix) Uzito wa Mzinga kuongezeka

x)Kijiti kuchomwa ndani ya Mzinga na kuona kama kina asali(Ukaguzi wa kienyeji)Njia hii haimuwezeshi mfugaji kujua kama asali imeiva ama mbichi.

xi)Sauti ya mzinga unapogongwa,inaashiria kama mzinga umejaa ama ni mtupu.

xii)Mwinamo wa mzinga kubadilika.
Muda wa Uvunaji asali baada ya kundi kuingia kwenye mzinga hutegemea mambo yafuatayo;
i)Kiwango cha maua yanayopatikana kwenye eneo la shamba la nyuki.

ii)Muda ambao maua hayo yanapatikana.

iii)Hali ya Hewa ya eneo hilo

iv)Ukubwa wa Kundi

v)Uwezo wa Nyuki kukusanya Nekta



KWA MAONI/USHAURI  
0768937884
fabianbalele@gmail.com




 

No comments:

Post a Comment