Monday, December 28, 2015

Mambo 10 Usiyoyajua Kuhusu Maisha ya "Nyuki"


1)Nyuki Malkia ni mkubwa kuliko Nyuki wengine katika kundi la Nyuki.
2)Nyuki Malkia ni jike pekee katika kundi la Nyuki mwenye uwezo wa kimaumbile wa kutaga mayai ingawaje kwenye kundi la Nyuki kuna majike wengi.
3)Nyuki Malkia ndiye Nyuki pekee mwenye uwezo wa kuishi muda mrefu zaidi,miaka mitatu hadi sita.
4)Nyuki VIBARUA ni majike ambao maumbile yao hayana uwezo wa kutaga mayai wala kujamiiana.
5)Nyuki dume hutokana na mayai ya Malkia yasiyorutubishwa na mbegu za kiume na kuwafanya nyuki hao kuwa na mzazi mmoja pekee yaani mama.
6)Nyuki dume hawana mshale wa sumu kwa ajili ya kujilinda dhidi ya maadui,badala yake wana uume.
7)Dume mmoja huweza kujaniiana na Malkia Mara moja tu ktk maisha take.
8)Baada ya tendo la kujamiiana Nyuki Dume hufa SAA chache kutokana na uume wake kukatika wakati wa kujamiiana.
9)Kwa hali hii,hata Nyuki vibarua hawajawahi kuwaona baba zao.
10)Kuna takribani aina tofauti elfu ishirini (20,000) za Nyuki wanaouma Duniani.



©Exclusive to "Balele Mwanahabari"..


Kwa maoni/Ushauri
0768937884 
fabianbalele@gmail.com

No comments:

Post a Comment