Thursday, January 17, 2013

ASASI ISIYO YA KESERIKALI(NON GOVERNMENTAL ORGANIZATION-NGO's)IITWAYO EXPERT'S ALLIANCE FOR COMMUNITY EMPOWERMENT-EACE YAANZISHWA.

     HONGERA KWA KUKAMILISHA       USAJILI.............
 Bwn. Fabian Balele Katibu Mtendaji wa EACE Akikabidhiwa Cheti cha Usajili wa Asasi isiyo ya Kiserikali iitwayo EXPERT'S ALLIANCE FOR COMMUNITY EMPOWERMENT-Makao makuu ya Ofisi za Wizara ya Maendeleo Ya Jamii Jinsia Na Watoto Jijini Dar es Salaam.

EXPERT'S ALLIANCE FOR COMMUNITY EMPOWERMENT(EACE) Ni Asasi isiyokua ya kiserikali inayodhamiria  kuiwezesha jamii ya Kitanzania kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma za Elimu Bora,Afya,msaada wa Kisheria,kuanzisha miradi mbalimbali,kupunguza maambukizi ya ukimwi,kujenga fursa za ajira,kuwawezesha wahitimu mbalimbali katika vyuo hapa nchini kupata ajira na huduma nyinginezo ili kupunguza umasikini na kuisaidia serikali katika kutekeleza sera mbalimbali zinazolenga kuisaidia jamii ya kitanzania.

EACE Ni Asasi inayowaunganisha wanafunzi mbalimbali wa vyuo vikuu hapa Tanzania wenye nia ya kuisaidia Jamii ya Kitanzania kwa kutumia Elimu,Ujuzi na Maarifa wanayoyapata kipindi cha masomo yao.

Akiongea kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro, Katibu Mtendaji wa Asasi hiyo Bwn. Fabian Balele  ameeleza kua mchakato mzima wa Usajili wa Asasi Hiyo umekwishakamilika ambapo Asasi ilisajiriwa Rasmi tarehe 03 JAN 2013 Makao makuu ya wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na watoto Jijini Dar-es-Salaam.

Alizidi kubainmisha kua Asasi hiyo imeanzishwa na wanachama 12 kutoka vyuo mbalimbali hapa Tanzania kama vile SUA,IFM,UDOM,CUHAS-BUGANDO,ARDHI.
Baada ya usajili mchakato wa kuwapata washiriki wengine kutoka vyuo mbalimbali unafanyika.
Kwa sasa Mchakato wa kupata FUNDS kwa ajili ya OFFICE unafanyika,kama ilivyobainishwa na Mwenyekiti wa Asasi iyo Bwn. Fransisi Msonge.
Afisa wa Usajili wa NGO's Wizara Ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Na Watoto Akiandaa Documents Muhimu tayari kwa  kumkabidhi Katibu Mtendaji wa EACE Bwn Fabian Balele Baada ya Kukamilisha Taratibu Za usajili Wizarani Hapo.

Makao makuu ya Asasi hiyo ni Jijini Mwanza.
Waweza kuwasiliana nao kupitia.

Email address, eacetanzania@gmail.com
Mobile no.   +255757979629- Chair  Person.

                      +255768937884-The Executive secretary
                       +255762446463-Treasury.

Tuesday, January 15, 2013

TRAFFIC UBUNGO TAFUTENI UFUMBUZI WA TATIZO HILI.

Tunamshukuru sana waziri wa Mawasiliano na uchukuzi Mh. Dk. Harryson Mwakyembe kwa juhudi kubwa anazozifanya kuhakikisha kuwa anawajibika ipasavyo ktk wizara yake ili kurahisisha shughuli za kimaendeleo za wananchi  wa Tanzania.

Waziri  Mwakyembe amekua mstari wa mbele kuhakikisha kua sekta ya uchukuzi inafanya kila juhudi ili kuatoa  huduma bora za uchukuzi
.
Kwa kuzingatia hilo Waziri Mwakyembe amekua akifanya ziara za kushtukiza Stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani ya Ubungo Jijini Dar es Salaam ili kujionea hali halisi ya huduma za usafiri mahali hapo.

Jambo kubwa ambalo amekua akilisisitizia ni kuhakikisha kua Abiria wanatozwa pesa za nauli stahili kulingana na safari husika na si vinginevyo.

Jambo lingine ni kuhakikisha kua Mabasi hayo yanakidhi vigezo mbalimbal vya safari ndefu .

Hata hivyo Askari wa barabarani wamekua wakiendesha zoezi hilo kwa kutumia mda mwingi sana kiasi cha kusababisha adha kubwa kwa abiria hasa waendao mikoani kutokana na kukaa ndani ya basi mda mrefu wakisubiri mabasi hayo kukaguliwa hasa nyakati za asubuhi..

Tunapenda kuwashauri Askari hao kubuni njia rahisi ya kukamilisha zoezi hilo kwa haraka zaidi ili kuepusha msururu mkubwa wa mabasi yaendayo mikoani hapo UBUNGO.

BAADHI YA MABASI YENDAYO MIKOANI YAKISUBIRI KUKAGULIWA NA ASKARI WA KIKOSI CHA BARABARANI-TRAFFIC katika Stand ya Mabasi ya UBUNGO Jijini Dar es Salaam kama yalivyokutwa na Balele Mwanahabari.