Monday, December 28, 2015

Mambo 10 Usiyoyajua Kuhusu Maisha ya "Nyuki"


1)Nyuki Malkia ni mkubwa kuliko Nyuki wengine katika kundi la Nyuki.
2)Nyuki Malkia ni jike pekee katika kundi la Nyuki mwenye uwezo wa kimaumbile wa kutaga mayai ingawaje kwenye kundi la Nyuki kuna majike wengi.
3)Nyuki Malkia ndiye Nyuki pekee mwenye uwezo wa kuishi muda mrefu zaidi,miaka mitatu hadi sita.
4)Nyuki VIBARUA ni majike ambao maumbile yao hayana uwezo wa kutaga mayai wala kujamiiana.
5)Nyuki dume hutokana na mayai ya Malkia yasiyorutubishwa na mbegu za kiume na kuwafanya nyuki hao kuwa na mzazi mmoja pekee yaani mama.
6)Nyuki dume hawana mshale wa sumu kwa ajili ya kujilinda dhidi ya maadui,badala yake wana uume.
7)Dume mmoja huweza kujaniiana na Malkia Mara moja tu ktk maisha take.
8)Baada ya tendo la kujamiiana Nyuki Dume hufa SAA chache kutokana na uume wake kukatika wakati wa kujamiiana.
9)Kwa hali hii,hata Nyuki vibarua hawajawahi kuwaona baba zao.
10)Kuna takribani aina tofauti elfu ishirini (20,000) za Nyuki wanaouma Duniani.



©Exclusive to "Balele Mwanahabari"..


Kwa maoni/Ushauri
0768937884 
fabianbalele@gmail.com

SIFA ZA SHAMBA LA NYUKI (MANZUKI)


Kuwapo Kwa mimea inayotoa Maua yanayotoa chakula cha nyuki cha kutosha, Kwa mfano,sehemu yenye misitu, shamba la miti au mazao ya kilimo. Muda wa mimea kuchanua ujulikane kwa mfugaji nyuki ili aweze kupanga muda ambao atawezesha kundi la nyuki kujijenga na kukusanya mazao ya kutosha wakati mimea inapochanua Maua. 

Maji ya kutosha ni muhimu, nyuki huyatumia kupooza kupooza joto ndani ya mzinga, kulainisha chakula na kurekebisha utamu wa asali ambayo hulishwa majana. 

Mahali panapofikia ili kuwezesha usafirishaji wa vifaa na mazao ya nyuki nyakati za uvunaji. 

Umbali wa kilomita tatu kutoka katika makazi ya watu,shule,hospitali na pasiwe mahali ambapo ni mapito ya Mifugo. Inapolazimu kuwa na Manzuki katika maeneo haya ,izungushiwe uzio wenye miti mirefu ili nyuki wanapokwenda nakurudi kutafuta cha kula wapiti juu  ili wasishambulie watu na wanyama. Umbali uliotajwa hapa ni kwa ajili ya nyuki  wanaouma tu. 

Mbali na maeneo ya kilimo kinachotumia kemikali kwa mfano kilimo cha tumbaku na korosho, Manzuki yaanzishwe umbali wa kilometa saba kutoka maeneo hayo. Hii ni kuzuia nyuki wasife kwa kemikali hizo, au kuzuia mizinga isiangushwe na pia kusababisha nyuki washindwe kurudi kwenye mizinga.
Kudhibiti uharibifu kutokana na maadui wa nyuki, wizi wa mizinga na mazao ya nyuki.

Viashiria Vifuatavyo hutumika sehemu mbalimbali kutambua muda wa kuvuna Asali..
i)Mwisho wa Msimu wa mvua na mwanzo wa Kangazi

ii)Maua au matunda ya mmea Fulani kupukutika

iii)Matunda ya mmea mwitu kutokeza

iv) Mazao ya shamabani kukomaa

v)Mng’urumo wa nyuki wakusanyao chakula kupungua

vi)Madume ya nyuki kuonekana yamekufa kwenye mlango ama chini ya mzinga

vii)Kundi la Nyuki kutanda nje ya Mzinga

viii)Gundi nyingi kuonekana katika mlango na matundu ya Mzinga

ix) Uzito wa Mzinga kuongezeka

x)Kijiti kuchomwa ndani ya Mzinga na kuona kama kina asali(Ukaguzi wa kienyeji)Njia hii haimuwezeshi mfugaji kujua kama asali imeiva ama mbichi.

xi)Sauti ya mzinga unapogongwa,inaashiria kama mzinga umejaa ama ni mtupu.

xii)Mwinamo wa mzinga kubadilika.
Muda wa Uvunaji asali baada ya kundi kuingia kwenye mzinga hutegemea mambo yafuatayo;
i)Kiwango cha maua yanayopatikana kwenye eneo la shamba la nyuki.

ii)Muda ambao maua hayo yanapatikana.

iii)Hali ya Hewa ya eneo hilo

iv)Ukubwa wa Kundi

v)Uwezo wa Nyuki kukusanya Nekta



KWA MAONI/USHAURI  
0768937884
fabianbalele@gmail.com




 

AINA ZA NYUKI NA TABIA ZAO


Nyuki ni jamii ya wadudu wenye jozi mbili za mabawa mepesi yenye mishipa laini.Nyuki huishi maisha ya kijamaa.Mwili wa Nyuki umegawanyika katika sehemu kuu tatu;kichwa ,kifua na tumbo(fumbati).Tofauti na wadudu wengine,nyuki hutengeneza na kuhifadhi Asali kwenye masega.

Kuna takribani aina tofauti elfu ishirini(20,000) Duniani.Nyuki hawa wanatofautiana kwa maumbile,ukubwa na tabia,lakini wote wanashahabiana kwa tabia moja ya kutembelea maua ili kukusanya mbochi(maji matamu yanayotengeneza asali) na chavua(unga unaopatikana kwenye maua) kwa ajili ya chakula chao.

Kuna jamii kuu mbili za Nyuki wanaopatikana Tanzania;Nyuki wanaouma na wasiouma.

NYUKI WANAOUMA
Nyuki wanaouma wanaopatikana Tanzania wamegawanyika katika makundi matatu kutegemea mahali wanapoishi.Wapo nyuki wanaoishi;
Sehemu za Mwambao(Pwani) wana umbo dogo na niwakali(Apis mellifera litorea),sehemu kame na tambarare,wana umbo la wastani,wakali kiasi na hutoa asali kwa wingi(Apis mellifera scutellata),sehemu za milimani,(zaidi ya futi 6,000 kutoka usawa wa Bahari) wana umbo kubwa na wapole,jina la kitaalamu wanaitwa Apis mellifera monticola.

NYUKI WASIOUMA
Nyuki wasiouma wanapatikana nchi za tropiki tu kama ilivyo Tanzania.
Nyuki wasiouma wanaishi ndani ya matundu ya miti,chini ya matawi makubwa ya miti,kwenye vichuguu vya mchwa na hata chini ya mapaa ya nyumba,nyuki hawa hu toa asali kidogo kulinganisha na nyuki wanaouma,Nyuki wasiouma wanaweza kutoa hadi lita 5 za asali kwa mwaka kutegemea na ukubwa wa mzinga,aina ,wingi wa nyuki na uwepo wa chakula(maua) cha kutosha.Asali ya Nyuki wasiouma inaaminika kuwa na uwezo mkubwa wa kutibu maradhi mablimbali kuliko asali ya Nyuki wanaouma.


JINSIA YA NYUKI NA MAJUKUMU YAO.
Kama ilivyo kwa viumbe vyote,nyuki nao waa jinsia mbili,nyuki dume na Nyuki Jike.Jinsia hizo ndiyo msingi wa mgawanyo wa majukumu ya kazi katika kundi la Nyuki.
Kundi la Nyuki wanaouma,lina aina tatu za Nyuki ambao ni Nyuki vibarua,malkia na dume.

NYUKI JIKE.
Jinsia hii inamakundi mawili ya nyuki amabyo hutekeleza majukumu mawili tofauti.

 a)Nyuki Malkia
NYUKI MALKIA(QUEEN)
Ni nyuki jike ambaye hulelewa kwa kula chakula rasmi(maziwa ya Nyuki) na kupata matunzo maalumu kwa maisha yake yote(tangu hatua ya yai hadi uzee wake wote)Chakula hiki humwezesha kuishi kati ya miaka miwili hadi sita.
Nyuki malkia ni mkubwa kuliko nyuki wengine katika kundi la Nyuki,tumbo lake ni refu lenye rangi ya njano na dhahabu ghafi.
Nyuki Malikia,hutoa kemikali(Pheremones)mwilini mwake kutoa miongozo  kwa kundi la Nyuki.Mpangilioo wote na Mgawanyo wa kazi katika kundi la nyuki hutegemea maelekezo yake.Kundi la Nyuki lisilo na Malkia hukosa mwelekeo na huishi kwa kipindi kifupi.

b)Nyuki Vibarua
Nyuki vibarua ni majike ambao maumbile yao hayana uwezo wa kutaga mayai wala kujamiiana na nyuki madume.Kwa kawaida nyuki vibarua ambao hawatagi mayai,ni majike tasaambao hawana uwezo wa wa kutaga mayai.Aidha,hufikia kuishi hadi siku 36.Wanaweza kufikia idadi ya 60,000 au zaidi katika kundi moja.

c)Nyuki dume
Hutokana na mayai ya Malikia yasiyorutubishwa na mbegu za kiumena kuwafanya nyuki hao kuwa na mzazi mmoja tu yaani mama,Nyuki dume ni wakubwa kuliko vibarua lakini wadogo kuliko Malkia.Macho yao ni makubwa na miili yao ina rangi nyeusi,nyuki dume hawana mshale wa sumu kwa ajili ya kujilinda dhidi ya maadui,badala yake wana uume.
Kazi kubwa ya Nyuki dume ni kujamiiana na malkia.Dume mmoja huweza kujamiiana na malikia mara moja katika maisha yake.,Baada ya Tendo la kujamiiana Dume hufa saa chache kutokan na uume wake kukatika wakati wa kujamiiana.

Kwa hali hii hata Nyuki vibarua hawajawai kuwaona baba zao.!

Kazi ya pili ya Nyuki madume ni kurekebisha hali ya hewa ndani ya mzinga kwa kupasha joto kiota hasa wakati wa Usiku kwa kukumbatia juu ya kiota,sehemu ya watoto.Wakati wa upungufu mkubwa wa chakula au kiangazi nyuki madume hutolewa na vibarua nje ya mizinga na baadea hufa kwa njaa au baridi.

Kwa Maoni/Ushauri
0768937884
fabianbalele@gmail.com