Saturday, December 22, 2012

OPTICAL MARK READER(OMR)-TEKNOLOJIA ILIYOSAIDIA KUPUNGUZA UDANGANYIFU MTIHANI DARASA LA SABA-2012.

Teknolojia mpya ya usahihishaji wa mitihani kwa kutumia kifaa cha kisasa(Optical Mark Reader) imechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza udanganyifu katika mitihanai ya darasa la saba iliyofanywa Septemba mwaka huu
.
Akiongea kutoka katika ofisi za Wizara ya Elimu jijini Dar Es Salaam,Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa amebainisha kua Teknolojia hii imepunguza udanganyifu katika mitihani hiyo kwa kua ni watahiniwa 293 pekee kati ya 865,534 waliofanya mitihani mwezi Septemba mwaka huu wamefutiwa matokeo yao ikilinganishwa na watahiniwa 9,736 waliofutiwa matokeo yao kutokana na sababu za udanganyifu kwa mwaka jana.
OPTICAL MARK READER
  MATOKEO YA DARASA LA SABA 2012.ASILIMIA YA UFAULU YAONGEZEKA.
Sanjali na hilo Pia Dk.Kawambwa alibainisha kua kiwango cha ufaulu wa darasa la saba umepanda Kwa asilimia 8.8(8.8 %) .

Hata hivyo matokeo hayo si mazuri sana kwani zaidi ya nusu ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza  mwaka 2013 wamepata Ufaulu wa daraja D.
Jumla ya wanafunzi 294,833 sawa na asilimia 52 % ya wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wamepata daraja D.
Ambapo wanafunzi 265,873 sawa na asilimia 47.41% walifaulu kwa viwango vya madaraja ya A,B,C.

Mchanganuo wa matokeo ya jumla kwa kufuata madaraja ni kama inavoonesha hapa chini
 Daraja.      Idadi ya Wanafunzi.
A                   3087
B                  40683
C               222,103
D               526,397.
E                  73,264
Jumla wa wahitimu 560,706 kati ya 865,534 wamechaguliwa kujiunga na Sekondari Jan.2013.
Kati yao wasichana ni 281,460-sawa na asilimia 50.20%
Wavulana ni 279,246 -sawa na 49.80%.











Dk.Shukuru Kawambwa,Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

No comments:

Post a Comment