Monday, December 3, 2012

VIJANA WASOMI WAASWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KTK MABADIRIKO YA KULINDA RASILIMALI ZA NCHI

Vijana wa vyuo vikuu wameaswa kua mfano ktk jamii ili kutetea na kulinda Rasilimali za nchi hii,kauli hizo zimetolewa na viongozi na Wabunge mbalimbali ktk Kongamano lililohusisha vijana wa CHADEMA vyuoni- Mkoani Morogoro,

Akiongea kwa masikitiko makubwa Mbunge wa Morogoro viti maalumu kwa tiketi ya CHADEMA Bi. Suzan Kiwanga,alidai kua viongozi wengi wa sasa wanajali maisha yao kwa kujilimbikizia mali na kuwasahau wananchi walio sehemu kubwa ya Taifa letu.

Nae Mbunge wa viti maaalumu wa Hanang, Manyara  Bi Rose Kamili aliwaomba vijana wa kike kushiriki ipasavyo katika masuala ya siasa kwani asilimia kubwa ya wasichana na wanawake kwa ujumla hawapendi siasa.

Alidai kua harakati za siasa haziepukiki kwani ktk nchi yetu bado tunamfumo wa kupata viongozi kupitia siasa na tusipokua makini wakati wa kuchagua viongozi watu wasiofaa watashika madaraka na kusababisha matatizo mbalimbali kwa kutokuwajibika.

Alizidi kusema kua vijana wajitokeze ktk kugombea nafasi mbalimbali za uongozi hasa udiwani kwani idadi kubwa ya madiwani ktk nchi hii hawana sifa za kuwawezesha kufanya maamuzi mazuri kutokana na elimu ndogo waliyo nayo.

Nae katibu wa BAVICHA(Baraza la Vijana Chadema)Taifa, Deo Munishi alielezea kwa undani kuhusiana na Falsa,Itikadi na Sera za CHADEMA na kuwaasa vijana kisoma kwa umakini katiba ya CHADEMA ili kuwaelimisha wananchi wa kawaida ambao wengi wao hawaijui katiba hiyo.

Aliendelea kwa kusema kua anasikitishwa na kitendo cha baadhi ya wanasiasa hapa nchini kwa kupotosha sera ya MAJIMBO ya CHADEMA kua ina lengo la kuwagawa Watanzania,Alidai kua kufikiri hivyo ni hali ya kua na upeo mdogo wa kufikiri kawani sera hiyo ina lengo la kuleta umoja na kuharakisha maendeleo kwa wanchi tofauti na baadhi ya wanasiasa ambao wamekua wakipotosha sera hiyo.
.
Nae Mchungaji Peter Msigwa a.k.a Mzee wa Falsafa mbunge wa Iringa Mjini  alidai kua vijana wajikomboe kifikra kwanza ndipo waweze kutaka kusimamia rasilimali za Taifa hili,aliongea kwa msisitizo huku akinikuu kauli mbalimbali za wasomi na wanafalsafa wa kale kama kama vile: "Problems can not be solved by the same level of thinking that created them"" Change what you think by changing what you see"

Alidai kua vijana kupitia CHADEMA hawatakua na maana yoyote iwapo watapata nafasi za uongozi na kuendelea kufanya madudu yale yale,vijana hasa Wasomoi wa chuo kikuu wanatakiwa kua chanzo cha kutafuta suruhisho la matatizo yanayowasibu wananchi wa kawaida na si kubaki kulalalamika  siku zote
.
Nae Mwenyekiti wa Bavicha Taifa-Ndg.JOHN HECHE alimalizia kwa kusema kua vijana wanatakiwa kujitoa kikamilifu ktk mapambano ya kupinga vitendo vya rushwa,tamaa ya madaraka,ubadhirifu,ufisadi na maovu mengine yaliyo kinyume na maadili ya Uongozi kwa nguvu zote kila siku bila kuogopa.

Kongamano hilo liliandaliwa na umoja wa vijana wa vyuo vikuu-CHADEMA(CHASO) kupitia Mkoa wa Morogoro.
                         Vijana kutoka SUA wakiwasili ktk hotel ya SARVOY  kwa ajili ya kushiriki ktk kongamano hilo.


viongozi wa CHASO(Morogoro)
Wakifatilia kwa makini mada zilizokua zikiwasilishwa ktk kongamano hilo.





Kulia-vijana kutoka vyuo mbalimbali wakifatilia kwa makini mada mbalimbali .
Kulia-Mbunge wa Hanang' Rose Kamili akiwasilisha mada ya mchango wa Vijana wa kike katika Siasa.
                   Mchungaji Peter Msigwa Mbunge wa Iringa mjini                akisisitiza jambo katika Kongamano hilo.
                                      John Heche-M/kiti BAVICHA akihitimisha kutoa mada katika kongamano hilo.
Kulia juu Mbunge wa Morogoro-CHADEMA,Bi Suzan Kiwanga,na Salvatory Machemli(kulia chini) mbunge wa Ukerewe wakimpongeza Balele Mwanahabari kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuihabarisha jamii ktk masuala mabalimbali.

No comments:

Post a Comment