Sunday, December 16, 2012

WATU KADHAA WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOANI SINGIDA KWA TUHUMA ZA KUTEKA GARI YENYE JENEZA LA MAREHEMU RYOBA MUNCHARI

Jeshi la Polisi mkoani Singida linawashikilia watu wapatao 25 kwa tuhuma za kuteka gari ndogo yenye maiti mali ya Chuo kikuu cha Sokoine(SUA) kilichopo mkoaniMorogoro.
.
Gari hiyo aina ya Land Cruiser iliyokua ikendeshwa na Bwn.Kastus Mapulila ilitekwa taehe 8/12/2012 kama ilivyoripotiwa na Balele Mwanahabari.

Akithibitisha kwa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi mkoani Singida Linus Sinzumwa amedai kua watuhumiwa hao wengi wao wanatoka kijiji cha Kisaki nje kidogo ya Manispaa ya Singida.

Aliendelea kuthibitisha kua baadhi ya mali zilizopatikana kwa watuhumiwa hao nio pamoja na laptop,kamera,simu za mkononi na nguo za wasindikizaji ktk msafara wa kusafirisha mwili wa Marehemu kuelekea Musoma mkoani Mara.
.
Inadaiwa kua watuhumiwa hao wamekamatwa kufuatia ushirikiano baina ya jeshi la polisi na wananchi baada ya watuhumiwa kulewa pombe na kudai kua wamepata pesa na hali zao kiuchumi zimeimarika.

Hatua za uchunguzi zinaendelea amabapo watuhumiwa watachujwa na baadhi kufikishwa mbele ya Sheria kujibu mashtaka yanayowakabili.

Jumla ya milioni 19 zilipokonywa katika tukio hilo la uvamizi wa msafara wa kusindikiza mwili wa Marehemu.

Marehemu Ryoba Munchari alikua mwanafunzi wa mwaka wa tatu kutoka chuo kikuu cha Sokoine(SUA)-Morogoro
Chanzo:Gazeti la Nipashe.

Gari iliyotekwa na majambazi huko Singida ikiwa imebeba mwili wa marehemu Ryoba Munchari mda mchache kabla ya safari kuanza kutoka Sua.

                                              Marehemu Ryoba Munchari enzi za uhai wake.
.

No comments:

Post a Comment