Saturday, November 17, 2012

MHADHARA WA KUMBUKUMBU YA HAYATI SOKOINE WAFANYIKA CHUO KIKUU CHA KILIMO SOKOINE MOROGORO

Makamu wa Rais Dr. Gharib Bilal alikua Mgeni rasmi na Msemaji mkuu  ktk Mhadhara wa 13 wa kumuenzi Hayati Moringe Sokoine uliofanyika jana tar 16 Nov.2012 Katika ukumbi wa Freedom Square ulioko chuo kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA)  Morogoro ktk CAMPUS ya Solomon Mahlangu.
Katika mhadhara huo,wageni mbalimbali na wanataaluma wakiwemo pia wanafunzi wa chuo hicho walipata nafasi ya kujumuika pamoja na kusikiliza hotuba iliyotolewa na Msemaji mkuu Dr. Gharib Bilal.
Miongoni mwa wageni hao alikua ni Mkuu wa chuo hicho(Al Noor Kassum) na makamu wake(Prof.Monela),wakuu mbalimbali wa idara za chuo,Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Naibu waziri wa Elimu,Mkurugenzi wa Elimu ya Juu na wengine wengi.
Katika hoyuba yake Dr. Bilal aliwaasa wasomi wa Tanzania kujichunguza kama kweli wanamuenzi Hayati Sokoine kwa vitendo na si nadharia.
Mmoja wa wanachuo aliyepata nafasi ya kumuuliza Msemaji mkuu wa mhadhara Dr. Bilal
Wanafunzi wa chuo hicho pia walipata nafasi ya kumuuliza msemaji mkuu Dr. Bilal maswali
mbalimbali.
Wanachuo kutoka SUA wakisikiliza hotuba ya Msemaji mkuu wa Muhadhara Dr.Galib Bilal
Makamu wa Rais Tanzania Bara Dr. Bilal akijibu maswali yaliyoulizwa na mmoja wa wageni ktk mhadhara huo
Prof fessor Ngaga,Dean of faculty of Forestry and Nature Conservation(katikati)Balele Mwanahabari(kushoto)na Mr.Gaston Buberwa mara baada ya mhadhara
Makamu wa Rais akipokea zawadi maalumu kutoka kwa Mkuu wa chuo hicho(Al Noor Kassum) ya bidhaa zinazotengenezwa ktk Chuo kikuu cha Sokoine,(baadhi ya bidhaa hizo ni kalamu,vitabu,T-shirts na kofia)
WANACHUO KUTOKA SUA

No comments:

Post a Comment